Monday, January 28, 2013

Wafanya biashara wa saruji wilayani karagwe walizwa na kupanda kwa bei ya bidhaa hiyo.




Wafanyabiashara wilayani karagwe hususani wanaojihusisha na uuzaji wa vifaa  vya ujenzi ikiwemo saruji na chokaa wamewaomba wateja wao kukubaliana na bei iliyopo ya vifaa hivyo  kwani  hubadilika kila wakati hii ni kutokana na  mfumuko wa bei  hapa nchini.


Wakizungumza na fadeco redio kwa nyakati tofauti  wafanyabiashara hao wamesema bei ya saruji imeshuka  ikilinganishwa na mwaka jana,huku wakitaja bei hizo kuwa
SARUJI aina ya simba imeshuka  kutoka sh:22,000/= hadi  sh:20,500/= Kwa wanunuzi wa jumla na sh:20,000/= kwa wale  wa rejareja.


Kwa upande  wa CHOKAA  aina ya Rhino imepanda  kutoka sh:14,500/= hadi  Sh:15,000/=  kwa bei ya rejareja.


Hata hivyo wafanyabiashara hao wabainisha baadhi ya changamoto wanazo kumbana nazo kuwa ni pamoja na bidhaa inapo panda  na kushuka bei wanapata hasara kwani wanakuwa wamenunua bidhaa nyingi,pia  mifuko kutoboka wakati wa kupakia na kupakua mizigo.

No comments:

Post a Comment