Saturday, January 19, 2013

WAZEE WAMEKUWA KITEGA UCHUMI KWA WENYE UWEZO.





WAZEE WAMEKUWA KITEGA UCHUMI KWA WENYE UWEZO.





Inakumbukwa mnamo tarehe mosi October 2010, waziri wa Jamuhuri ya Muungano Wa Tanzania Mizengo Kayanza Peter Pinda kupitia hotuba yake katika mahadhimisho ya siku ya wazee duniani aliseme matibabu bure kwa wazee halina mjadala.


Alisema hayo katika uwanja wa Jamuhuri mkoani Morogoro.
Tangu kutolewa kwa tamko hilo mashirika yasiyokuwa ya kiserikali yamelivalia njuga na kuunganika na mashirika yanayohudumia wazee nchini ili kuunganisha nguvu na sauti za pamoja za wazee kudai haki na stahiki zao.


Pamoja na juhudi za mashirika hayo yapo mashirika bandia yaliyoibuka kupitia migongo ya mashirika hayo kuwarubuni wazee kuchangia  fedha ambazo hazikuwa na viwango maalum  wakidai kuwapatia huduma ya Afya bure, pensheni na huduma nyingine zinazodaiwa na wazee kutoka serikali ya Tanzania.


Hata hivyo matatizo ya wazee   yamebaki pale pale kwani waliochukua fedha za wazee hao na kuwaorodhesha hawakurudi tena.


Kutokana na vitendo hivyo kuripotiwa kujitokeza sehemu mbalimbali hapa mkoani Kagera shirika la SAIDIA WAZEE KARAGWE {SAWAKA}  kupitia kwa mwenyekiti wake Mzee Nekemia Kazimoto LIMETOA RASMI TAMKO KWA MASHIRIKA HAYO HEWA  kuwa haliyatambui mashirika hayo.


Taarifa hiyo kwa vyombo vya habarri imeeleza kuwa  shirika la SAWAKA limepokea malalamiko toka kwa wazee katika sehemu mabalimbali za wilaya ya Karagwe na Kyerwa, wakilalamikia kuwa wamerubuniwa na baadhi ya watu toka shirika lisilojulikana ambalo limeanza hivi karibuni kwa kuwatoza wazee shs 2,500/= kwa kuwapatia vitambulisho vya kuwatambulisha wazee kwa ajili ya matibabu na huduma mbalimbali bure toka serikalini.
  

Na  kwamaba wazee hawa wamekuwa wakivipeleka vitambulisho hivyo katika vituo vya Afya na Hospitali kama vile Nyakahanga na kufukuzwa kwani havina uhalali na havikutolewa na mamlaka husika.


Hivyo wazee na jamii inayowahudumia imewekwa wazi kuwa Vitambulisho vya wazee vinavyotolewa na shirika hilo havina uhalali wowote kwani havina baraka za serikali na havitambuliwi na mamlaka husika na havina anuani wala muhuri wa wahusika kuthibitisha uhalali wake.


Shirika la SAWAKA  linawaakikishia wananchi woto karagwe na  Kyerwa kwamba haina uhusiano wala ushirikiano wowote na kundi hilo au shirika husika.


Katika ufuatiliaji wake wamebaini  kuwa hakuna shirika au Asasi iliyo hai ijulikanayo kama῝wazee wa Taifa la Tanzania῞ ambayo imepewa jukumu la kutoa vitambulisho hapa nchini  na kuongeza kuwa kama lipo ndizo zile Asasi za mfukoni ambazo zinatia doa shughuli za kazi nzuri za NGO’s.


Kwa tamko hilo Wazee wanatahadharishwa kutochukua vitambulisho hivyo kwani vinatia mashaka sana na kuwataka viongozi wa matawi ya SAWAKA yaliyopo vijijini kuwaelimisha wazee kuwa na subira ya kupata vitambulisho vya mapema mwaka huu kama serikali ilivyokwisha toa ahadi.



Taarifa hiyo imesema kuwa Vitambulisho hivyo bandia kwa wazee vimeanza kutolewa katika wilaya za Karagwe hasa Nyakahanga, Kihanga, Chanika, Nyaishozi, na Ihembe,ambapo wasi wasi mkubwa ni kwamba huenda  kundi hilo likaendeleza mchezo huu katika wilaya  jirani za Muleba, Misenyi na Bukoba.



Wayaomba  mashirika ambao ni washirika wao  wanayofanya nayo kazi kma TUWAMI, NA KWA WAZEE kuwaelimisha wazee kuhusu utapeli huu ambao unaonekana kuwa mradi wa watu wachache wanaotafuta kujinufaisha na fedha za wazee.



SAWAKA kwa kushirikiana na Halmashauri ya wilaya ya Karagwe na Kyerwa, imewomba wazee kuvuta subira kuwa watatioa taarifa juu ya utaratibu utakaotumika pindi serikali itakapokamilisha mchakato huo.



Suala hili  limefikishwa serikalini  na kuthibitisha kuwa vitambulisho hivyo ni bandia na kutoa taarifa kwa vyombo husika ili wahusika wakamatwe  na kuchukuliwa hatua  za sheria huku wazee wakiombwa  kutoa ushirikiano wa kuwabaini wanaotoa vitambulisho hivyo bandia  kwa wazee.

No comments:

Post a Comment